November 4, 2015



Kocha Mkuu wa Yanga, Mholanzi, Hans VanDer Pluijm, amekiri ugumu wa ubingwa wa Ligi Kuu Bara, lakini amepanga kupambana kuhakikisha anashinda kila mchezo atakaocheza.
Kauli hiyo, ameitoa hivi karibuni baada ya kufanya tathmini nzima ya ligi kuu katika mechi tisa walizozicheza baada ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kusimamisha ligi hiyo ili kupisha kambi ya Taifa Stars.

Timu hiyo, hadi hivi sasa tayari imecheza michezo tisa, kati ya hiyo, imetoka sare michezo miwili dhidi ya Azam FC mabao 1-1 na Mwadui FC 2-2 huku hiyo mingine ikishinda.
Akizungumza na Championi Jumatano, Pluijm alisema kwa jumla ligi kuu ni ngumu kwa upande wao kutokana na kila timu wanayokutana nayo kucheza soka la fujo na kulinda lango lao dakika zote 90.

Pluijm alisema, hilo ameliona tayari na amepanga kulifanyia kazi mara ligi kuu itakapoanza tena kwa kuhakikisha anawapa mbinu wachezaji wake za kuhakikisha wanashinda kwa kila mechi watakayoicheza.

Aliongeza kuwa, watakuwa wanawalazimisha wachezaji wa timu pinzani kutoka langoni  kutokana na kushambulia kila wakati kwa ajili ya kuwachosha.

“Moja ya tahadhari nitakayoingia mara baada ya ligi kuu kuanza ni kuwataka wachezaji wangu kucheza kwa umakini mkubwa kwenye mechi zote kwa kuhofia majeruhi kikosini kwangu.

“Hiyo ni kutokana na timu pinzani kucheza soka la fujo kwa kuwachezea rafu za makusudi wachezaji wangu, ninaamini kama wachezaji wangu wakipata majeraha, basi malengo yangu hayatatimia.

“Pia nimepanga wachezaji wangu kucheza soka la kushambulia dakika zote kwenye lango la timu pinzani, hiyo ni kutokana na kila timu tunayokutana nayo kulinda lango lao,” alisema Pluijm.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic