November 4, 2015


Mechi kati ya Azam na Toto Africans ya Mwanza uliopigwa wikiendi iliyopita uliweka rekodi ya aina yake baada ya kuwa pambano lililopigwa kwa muda mrefu zaidi katika mechi zote za ligi mpaka sasa.


Pambano hilo lilimalizika kwa Azam inayonolewa na Muingereza, Stewart Hall, kuibuka na ushindi wa mabao 5-0, rekodi hiyo ni mechi kuchezwa kwa dakika 111 ikiwa ni zaidi ya dakika 21 za muda wa kawaida.

Kisa cha pambano hilo kupigwa kwa muda wote huo ni kutokana na wachezaji wa Azam kupata madhara wakati mechi ikiwa inaendelea ambapo wachezaji Jean Mugiraneza na kipa Aishi Manula waliomba udhuru wa kwenda maliwatoni pamoja na kipa wa Toto, Mussa Mohammed, kutumia muda mrefu akifanyiwa matibabu.

Kipindi cha kwanza cha pambano hilo baada ya kufika dakika 45 za mapumziko mwamuzi wa mezani alionyoosha dakika tisa za nyongeza na katika kipindi cha pili baada ya kufika dakika 45 mwamuzi huyo alinyoosha dakika 12 za kuendelea mchezo huo akifidia muda ambao ulitumiwa na wachezaji hao kwenda msalani.

Katika rekodi ya Ligi Kuu Tanzania Bara kwa siku za hivi karibuni, hakuna mechi ambayo imechezwa kwa muda mrefu hivyo au wachezaji wawili kwenda msalani wakati mchezo ukiendelea.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic