November 8, 2015


Na Mwandishi Wetu, Johannesburg
Kikosi cha Taifa Stars leo kitapumzika kwa siku moja baada ya mazoezi ya siku sita mfululizo.

Kocha Charles Boniface Mkwasa ameamua vijana wake wapumzike kabla ya kufanya mazoezi mengine kesho katika Uwanja wa Edenvale jijini Johannesburg.

Baada ya mazoezi ya kesho, Stars itakuwa na mechi ya kirafiki dhidi ya timu ya taifa ya Afrika Kusini chini ya miaka 23 itakayopigwa Jumanne.

“Mapumziko ni Jumapili, pia wachezaji watapata muda wa kutembea kidogo hapa na pale. Baada ya hapo tutarejea tena mazoezini Jumatatu,” alisema Mkwasa.

Stars inajiandaa na mechi dhidi ya Algeria kuwania kucheza Kombe la Dunia 2018 nchini Urusi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic