November 6, 2015


Na Saleh Ally, Johannesburg
KOCHA Mkuu wa Taifa Stars, Charles Boniface Mkwasa jana aliungana na baadhi ya wataalamu wa masuala ya soka nchini hapa kuangalia baadhi ya mechi za Algeria.


Stars inajiandaa kuivaa Algeria Novemba 14 jijini Dar es Salaam katika harakati zake za kuwania kucheza Kombe la Dunia.

Mkwasa aliamua kufanya hivyo akiungana na baadhi ya memba wa benchi la ufundi kama Abdallah Kibadeni na Juma Mgunda, kuangalia namna Algeria wanavyopambana.

Mkwasa akiwa na memba hao na baadhi ya wataalamu wa soka Afrika Kusini walioalikwa, waliangalia pamoja.

“Tunaangalia kwa ajili ya kujifunza mambo mbalimbali. Soka ni mchezo wenye mambo mengi ikiwa ni pamoja na kujifunza kupitia kwa wenzako.

“Lengo ni kujua Algeria wana mipango ipi, mfano tofauti ya mipango ya nyumbani na ugenini na nini cha kufanya,” alisema.


Stars jana ilifanya mazoezi mara mbili kwenye Uwanja wa Edenvale jijini hapa ikiwa ni sehemu ya kuendelea kujifua.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic