November 6, 2015


Na Saleh Ally, Johannesburg
KIKOSI cha Taifa Stars kilichoweka kambi nchini hapa kimeandaliwa mpishi maalum.

Pamoja na ubora wa hoteli ya Holiday Inn waliyofikia, lakini Stars wamewekewa mpishi huyo.

Mratibu wa Taifa Stars, Msafiri Mgoyi amesema lengo ni kuhakikisha wachezaji wanakula chakula sahihi na wanachohitaji.

“Wakati mwingine hata chakula ni utamaduni. Lakini mpishi anayekuja hapa ni yule ambaye anajua kupiga hata ugali.

“Wachezaji watakula wanachotaka na kwa wakati mwafaka. Kingine bado ni umuhimu wa suala la usalama,” alisema Mgoyi.

Stars inajiandaa kuivaa Algeria Novemba 14 jijini Dar es Salaam katika harakati zake za kuwania kucheza Kombe la Dunia.

Kikosi hicho chini ya Charles Boniface Mkwasa kinahitajika kushinda mechi ya kwanza na kujiwekea mazingira mazuri kabla ya mechi ya pili Novemba 17, ugenini.

Kikosi cha Taifa Stars kimefanya mazoezi leo Asubuhi, pia kitaendelea kufanya jioni.

Mazoezi yamefanyika chini ya Kocha Charles Boniface Mkwasa ambaye ana wasaidizi wengine kama Hemed Morocco na Juma Mgunda pia mshauri wa masuala ya Ufundi, Abdallah Kibadeni pamoja na Kocha wa Makipa, Manyika Peter.
Meneja ni Omary Kapilima.

Mazoezi yamefanyika kwenye Uwanja wa Edenvale kwenye kitongoji cha Edenvale jijini Johannesburg, Afrika Kusini.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic