November 6, 2015

KAMBI YA TAIFA STARS JIJINI JOHANNESBURG, AFRIKA KUSINI

Na Saleh Ally, Johannesburg
KAMBI ya Taifa Stars iko katika hoteli ya Holiday Inn jijini hapa na ulinzi ni mkali hasa.

Mazingira ya kambi hiyo yako katika utulivu sana na uzio wote umezungushiwa nguzo za umeme.


Anayeingia lazima anahojiwa na askari zaidi ya wanne ambao wanakuwa kwenye lango kuu la kuingilia.

Hata akiingia analazimika kuyapita majengo matatu kabla ya kufikia hoteli iliyo.

Hakuna sehemu yoyote ya karibu kwa ajili ya vinywaji au mtu anaweza kwenda kutembelea, badala yake hata kama ni maji au mahitaji ya ziasa ya wachezaji angalau takribani kilomita 2 yanaweza kupatikana.

Mratibu wa Taifa Stars, Msafiri Mgoyi amesema wamefanya hivyo ili kuweza kufikia malengo.

“Hii ni timu ya taifa, suala la usalama ni la kwanza. Lakini tunaangalia utulivu pia na kuhakikisha wachezaji wanapumzika,” alisema.


Stars inajiandaa kuivaa Algeria Novemba 14 jijini Dar es Salaam katika harakati zake za kuwania kucheza Kombe la Dunia. Mechi ya marudiano itachezwa Novemba 17 jijini Algers.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic