November 3, 2015

Wachezaji wa Yanga wamepewa mapumziko ya siku 10 kabla ya kurejea kazini.

Kocha Mkuu, Hans van der Pluijm ameamua kutoa ofa hiyo kwa wachezaji wake kutokana na ligi kusimama.

Hata hivyo wachezaji hao wametakiwa kurejea kazini Vovemba 12 kuanza kujifua.

Meneja wa Yanga, Hafidhi Saleh amesema kikosi hicho kitaanza kujifua Novemba 12 isipokuwa wachezaji walio katika kikosi cha timu ya taifa, Taifa Stars kitakachocheza Novemva 14 dhidi ya Algeria.

“Wale walio katika timu ya taifa ya wanaocheza Novemba 14, pia watakaokwenda katika timu nyingine za taifa.

“Tutaanza mazoezi taratibu na baada ya wale walio katika vikosi vya taifa, wataungana na wenzao na kuendelea na programu,” alisema Saleh.


Baada ya mechi 9, Yanga ambao ni mabingwa watetezi wamebaki katika nafasi ya pili katika msimamo wa Ligi Kuu Bara wakiwa na pointi 23 nyuma ya vinara Azam FC wenye 25.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic