November 9, 2015

MAYANJA (KULIA)

Huku kukiwa na hali ya sintofahamu kwa timu ya Coastal Union kama ni kumtosa au kuendelea na Mganda, Jackson Mayanja kuinoa timu hiyo, ghafla Kiyovu Sports ya Rwanda imeibuka na kutaka huduma ya kocha huyo.

Mayanja ambaye amekosa matokeo mazuri kwenye mechi za awali za Coastal, amekuwa akihusishwa kuvunjiwa mkataba na timu hiyo lakini uongozi umekuwa ukikosa jibu la moja kwa moja kuhusiana na ishu hiyo.

Mmoja ya marafiki wa karibu na kocha huyo aliyepo Uganda kwa sasa akimuuguza mama yake, amesema kuwa Kiyovu wamempigia simu na kumueleza dhamira yao lakini bado hawajakubaliana moja kwa moja.

“Zipo timu mbili zinamtaka, lakini Kiyovu ndiyo wamempigia simu, yeye (Mayanja) amewaambia kwamba wasubiri kwanza amalize kumuuguza mama yake ambaye amefanyiwa upasuaji wa tumbo hivi karibuni, baada ya hapo watazungumza, maana anaheshimu mkataba wa Coastal pia,” kilisema chanzo hicho.

Alipotafutwa Mayanja kuzungumzia suala hilo, alisema kwa kifupi: “Nani amekwambia? Ni kweli Kiyovu nimewasiliana nao lakini hatujafikia popote, maana bado nipo ndani ya mkataba na Coastal kwa sasa.”


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic