December 15, 2015


Kiungo wa zamani wa Barcelona na Real Madrid, Luis Figo amesema Cristiano Ronaldo anaweza kuwashangaza watu na kushinda tuzo ya Ballon d’Or.

Figo aliyewahi kushinda tuzo hiyo mwaka 2000 akiwa Barcelona amesema bado Ronaldo ana nafasi licha ya kuingia fainali dhidi ya Lionel Messi na Neymar, wote kutokea Barcelona.

“Upigaji kura wa tuzo ni mtu mmojammoja, huwezi kujua mtu kavutiwa na ubora wa mabao au kitu kingine.

“Lolote linawezekana, Ronaldo anaweza kuwa ndiyo mshindi na watu wengi wakashangaa,” alisema Figo.


Ronaldo ni mshindi wa Ballon d’Or kwa mara tatu akianza na mwaka 2008 akiwa na Man United, halafu mwaka 2013 na 2014 akiwa na Real Madrid.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic