December 19, 2015


Tena kwa kushitukiza, hali ya hatari imetangazwa kwa timu yoyote itakayokutana na JKT Ruvu inayonolewa na Kocha Abdallah Kibadeni katika mechi za Ligi Kuu Bara kuwa ni lazima ifungwe.

Kibadeni ametoa kauli hiyo huku kesho Jumapili timu yake ikicheza na Coastal Union kwenye Uwanja wa Karume, Dar es Salaam katika muendelezo wa ligi kuu.

Alisema; “Ninachoangalia sasa katika ligi ni kushinda kila mechi bila ya kujali tunakutana na timu yenye kiwango kipi, sisi hatujali hapa yeyote anayekuja mbele yetu tutahakikisha tunamfunga.


“Ushindi tulioupata wikiendi iliyopita dhidi ya Prisons (mabao 4-0) ni ishara kuwa kikosi kinaonyesha mwanga wa mafanikio,” alisema. JKT Ruvu na Coastal Union zote zina pointi nane lakini Coastal ipo juu katika nafasi ya 13 kwani ina tofauti kubwa ya mabao kuliko JKT iliyo nafasi ya 14.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic