December 14, 2015

 Mshambuliaji Donald Ngoma wa Yanga amerejea mazoezini na matumaini makubwa atacheza mechi ya Jumatano dhidi ya African Sports.

Katika mazoezi yaliyofanyika kwenye Uwanja wa Shule ya Sekondari ya Garanosi mjini Tanga, leo. Kocha Hans van der Pluijm alionekana kuwa naye karibu akimfundisha mambo kadhaa, hali 
inayoonyesha amerejea.


Yanga ilimkosa Ngoma ambaye alikuwa majeruhi katika mechi yake dhidi ya Mgambo iliyoisha kwa sare ya bila bao, juzi. 

Kurejea kwake itakuwa ni sehemu ya kufufua matumaini ya kupata pointi zote tatu dhidi ya African Sports ambao wameishatamba hawana hofu na Ngoma pia Yanga kwa ujumla.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic