December 14, 2015


Mshambuliaji nyota wa TP Mazembe na Tanzania Mbwana Ally Samatta ameweka rekodi nyingi mpya baada ya leo kutangazwa kuingia fainali ya kuwania tuzo za mwanasoka bora Afrika  kwa wanaocheza ndani ya bara hili 2015
Samatta ni mfungaji bora wa Ligi ya Mabingwa Afrika, ameingia na vigogo wengine lakini bado anaweza kuwa na nafasi ya kutwaa tuzo hiyo.
Fainali au wachezaji waliongia hiyo tatu bora kwa wanaocheza Afrika ni Baghdad Boundjah (Algeria/ Etoile du Sahel-Tunisia), Mbwana Ally Samatta (Tanzania/ TP Mazembe-Congo DR), na Robert Kidiaba (DRC/ TP Mazembe-Congo DR).
Kwa upande wa walioingia fainali wanaowania tuzo hiyo kwa Afrika hasa wanaocheza nje ya bara hili ni;
Andre Ayew (Ghana/ Swansea City-England), Pierre-Emerick Aubameyang (Gabon/ Burussia Dortmund-Ujerumani) na Yaya Toure (Ivory Coast/ Manchester City-England).

Kwa sasa Samatta yuko nchini Japan akiitumikia TP Mazembe katika michuano ya klabu bingwa ya dunia.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic