December 9, 2015


Kikosi cha TP Mazembe kipo katika mji wa Osaka, Japan ambako kitacheza mechi zake mbili za kwanza za Kombe la Dunia.


Mabingwa hao wa Afrika wamefikia katika hoteli ya Intercontinental ambayo ni moja ya hoteli bora kati ya hoteli bora kabisa 170 duniani.

Ili kuonyesha Wajapani wanajua biashara, walichoamua ni kubadilisha baadhi ya rangi za vyumba vya hoteli hiyo na kutumia nyeusi na nyeupe kwa heshima ya TP Mazembe.

Meneja wa TP Mazembe, Frederic Kitenge ameonekana kuridhishwa kabisa na hali ya utulivu na ubora wa hoteli hiyo ambayo mabingwa hao wakiwemo Watanzania wawili, Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu, wamefikia hapo.




0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic