December 19, 2015


Yanga imeanza kujifariji eti uwezo wa kiungo mshambuliaji wake mpya, Issofou Boubacar raia wa Niger ni sawa na ule wa nyota wa zamani wa Simba, Emmanuel Okwi.

Kauli hiyo imekuja baada ya baadhi ya wadau wa soka nchini kuponda uwezo wa Bobacar anayemudu kucheza winga za kulia na kushoto pia kiungo cha ushambuliaji kuwa hana jipya kikosini.

Yanga imemsainisha Boubacar mkataba wa mwaka mmoja katika dakika za mwisho, usajili ambao umeonekana kuwa na shaka huku ikionekana kuwa mchezaji huyo hakuwa akipata nafasi alipokuwa akicheza Esperance ya Tunisia.

Katibu Mkuu wa Yanga, Dk. Jonas Tiboroha amesema kuwa: “Nashangaa baadhi ya watu wanaomponda Boubacar, kukaa benchi ni kitu kingine lakini mimi naamini ana uwezo kama wa Okwi tu.”

“Ukimtazama vizuri utaona Boubacar ana kasi na mbinu nyingi kama zile za Okwi, yaani huyu anafanana sana na Okwi hakuna ubishi katika hilo na watu watamuona siku akicheza.”


Alisema katika soka kuna vitu vingi na ndiyo maana Boubacar hakupata nafasi Esperance lakini anaamini atafanya vizuri akiwa Yanga wakati huu.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic