January 7, 2016


Kocha Mkuu wa timu ya Taifa ya Wanawake ya Mpira wa Miguu (Twiga Stars), Rogasian Kaijage amejiuzulu nafasi hiyo kuanzia leo baada ya kuomba kwa uongozi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu  nchini (TFF).

Kaijage aliiongoza Twiga Stars kwenye fainali za michezo ya Afrika (All Africa Games) zilizofanyika nchini Congo Brazzavile Septemba mwaka jana, baada ya kuiondoa timu ya taifa ya Zambia katika hatua ya mtoano.

TFF imesikitishwa na taarifa za kujiuzulu kwa kocha huyo mwenye leseini A ya CAF, ambaye amekuwa akizinoa timu za taifa za wanawake ya wakubwa (Twiga Stars) pamoja na timu ya wanawake wenye umri chini ya miaka ya 20 (Tanzanite) tangu mwaka 2013.

Kufuatia kujiuzulu kwa kocha Kaijage, TFF inaendelea na programu za maendeleo ya soka kwa wanawake, ikiwemo kuendesha ligi ya wanawake (Tanzania Women League).

TFF inamtakia kila la kheri kocha Rogasian Kiajage katika shughuli zake.

Aidha maandalizi ya mchezo kati ya Twiga Stars dhidi ya Zimbambwe  yataendelea chini ya kocha atakayeteuliwa kuchukua nafasi yake, mchezo utakaochezwa mwezi Machi mwaka huu na mshindi kucheza na Zambia.


TFF  itaendelea kupambania kwenye maendeleo ya soka la wanawake.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic