March 27, 2016


Shirikisho la Soka Africa (Caf), limetangaza kuiondoa Chad katika michuano ijayo kuwania kufuzu kucheza Afcon na mingine yote iliyo chini yake.

Kama hiyo haitoshi, Caf imetangaza kuitwanga Chad faini ya dolla 20,000 (zaidi ya Sh milioni 44) kutokana na kitendo chake cha kujiondoa katika michuano ya ya kuwania kucheza Afcon.


Chad ilitarajiwa kucheza kesho dhidi ya Taifa Stars kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam baada ya kuwa imetwangwa bao 1-0 kwao ND’jamena.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic