March 28, 2016


RAIS WA TFF, JAMAL MALINZI (KUSHOTO) AKIWA NA RAIS WA CAF, ISSA HAYATOU

Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), kesho linaanza kurudisha fedha za mashabiki waliokata tiketi kwa ajili ya mechi kati ya Taifa Stars dhidi ya Chad iliyokuwa ipigwe leo.

Mashabiki waliokata tiketi kwa ajili ya mechi hiyo ya kuwania kucheza Afcon kuahirishwa.

Kwa mujibu wa TFF, fedha hizo zitaanza kurudishwa kesho katika vituo watu walipokata tiketi hizo.


“Kikubwa kila mtu aende na tiketi yake sehemu aliyokatia arudishiwe fedha yake,” alisema Jamal Malinzi, Rais wa TFF.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic