April 18, 2016


Straika wa Arsenal, Welbeck.

Mshambuliaji wa zamani wa Newcastle United, Alan Shearer ambaye kwa sasa ni mchambuzi wa soka amewaambia Arsenal kuwa hawawezi kutwaa ubingwa wa Premier League mpaka pale watakaposajili straika wa daraja la kwanza ‘world class striker’.

Nahodha huyo wa zamani wa England alisema hayo alipokuwa akifanya kazi yake ya uchambuzi baada ya Arsenal kupata sare ya bao 1-1 dhidi ya Crystal Palace, jana Jumapili.
 
Alan Shearer
“Hawawezi kutwa ubingwa wa ligi mpaka watakapo msajili straika wa kiwango cha juu ambaye anaweza kufunga mabao 25 au 30 katika msimu mmoja,” alisema Shearer ambaye alifunga mabao 260 katika Premier League enzi zake alipokuwa akicheza idadi ambayo hajawahi kufikiwa na mchezaji mwingine yeyote.

“Nimekuwa nikisema hivyo msimu wote kuwa wanatakiwa kuwa na angalau wachezaji wawili wenye ubora huo na maoni yangu nana yanaonekana mpaka sasa,” aliongeza.

Kauli hiyo ni kama mwiba kwa washambuliaji wa timu hiyo akiwemo Mwingereza, Danny Welbeck.
 
Yannick Bolasie wa Crystal Palace akifunga bao la kusawazisha, jana.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic