April 12, 2016

BAWAZIRI AKIHOJIWA NA BARUAN MUHUZA WA AZAM TV


Kaimu Katibu Mkuu wa Coastal Union, Salim Bawaziri amesema wana kila sababu ya kubeba Kombe la FA.

Coastal Union imepangwa na Yanga katika mechi ya Kombe la Shirikisho ambayo itapigwa Aprili 24 mjini Tanga.

“Watu watofautishe Kombe la Shirikisho na Ligi Kuu Bara. Kwenye ligi hatufanyi vizuri lakini Shirikisho hakuna mjadala, tunachukua.

“Hao Yanga wanajua kwamba wanaanzia Mkwakwani ambako ni machinjioni, hakuna mjadala watakwisha pale,” alitamba.

Coastal imevuka baada ya kuiangusha Simba na kuweka rekodi ya kuwa timu iliyozifunga Yanga, Azam FC na Simba ndani ya dakika 90 kwenye Ligi Kuu Bara na Kombe la Shirikisho.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic