June 16, 2016



Beki wa Yanga, Vicent Bossou ametua mjini Antalya nchini Uturuki na kuungana na wenzake.

Bossou ametua nchini humo katika kambi ya Yanga ambayo inatarajia kuondoka kesho kwenda Algeria kuivaa Mo Bejaia katika mechi ya Kombe la Shirikisho hatua ya robo fainali.


Beki huyo raia wa Togo alichelewa kujiunga na wenzake kutokana na matatizo ya kifamilia nchini Ivory Coast ambako ndiyo asili yake.

Alichofanya ni kuja hadi Dar es Salaam, halafu akaanza safari ya kwenda Antalya nchini Uturuki kuungana na wenzake na kesho ndiyo safari ya kwenda Algeria.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic