September 10, 2016



MAMA wa Miss Tanzania 2016, Wema Sepetu, Bi. Miriam Sepetu ameingia kwenye headlines mitandaoni baada ya kutofautiana na mkali wa nyimbo za singeli, Man Fongo.
Kwa mujibu wa Man Fongo akihojiwa na baadhi ya vyombo vya habari amekiri kutokea kwa mfarakano huo huku akisisitiza kuwa hajatenda kosa lolote kwa mama Wema.
“Hii ilianza wakati akiwa safarini na wasanii wenzake wakitoka Kahama kwenda wilayani Mureba kufanya shoo ya fiesta. Wakiwa kwenye gari,”
“Christian Bella akanza kwa kusema kuwa kila anapoposti kitu chochote mtandaoni anatukanwa.”
Ndipo Man Fongo akauliza, “Unatukanwa na nani na kisa ni nini?”
Maelezo yaliendelea kutolewa na Bella huku wasanii wengine wakichangia hiyo maada na baadaye maada ikawa imeisha.
Kwa mujibu wa Man Fongo anadai baadaye alitumiwa ujumbe wa matusi kwenye simu yake na mama Wema huku akishutumiwa kuzungumza maneno machafu yenye nia ya kuichafua familia ya Sepetu.
Msikie Man Fongo: “Wamemtumia meseji mama yake na Wema kwamba ninaisema familia yake wakati mimi Manfongo muhuni na muhuni siku zote hatuna muda wa kumzungumzia mtu, riziki yangu naisaka tangu nipo kitaani sina muda wa kujibishana na watu sasa Mama Wema ananitumia meseji za matusi”
Msikie Mama Wema:Kwanza kama utakuwa umesoma SMS yangu niliyomtumia nilimwambia kwamba Amani nakuheshimu sana hasa baba yako ambae mpaka sasa namuheshimu ila matusi ambayo umeanza kunitukana huko ulipo nimeyapata sasa endelea…..”
“Sasa mimi ndio wakumshtaki maana amenisema vibaya huko walipokuwa na watu wake ziarani nimeumia sana mimi kama mzazi, Manfongo bado  mtoto mdogo sana kwangu na mimi”..
Bonyeza play kuitazama hii video Mama Wema Sepetu akieleza tofauti yake na Man Fongo

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic