October 12, 2016



Mliokuwa hamjazaliwa someni hiyo historian
Rais Jaffery Nimeiry wa Sudan akikagua wachezaji waTaifa Stars waliokuwa vifua wazi. Kapten Abrahaman Juma akimtambulisha kwa Omary Zimbwe, Mohamed Chuma, Kitwana Manara na Abdalla KIbadeni. Rais J. K. Nyerere alikuwa Jukwaa Kuu.

"Jezi za Taifa Stars zilikuwa zimepelekwa kwa Mganga wa Kienyeji ili ishinde. Siku ya mechi, Meneja wa Taifa Stars alizifuata lakini bahati mbaya hakumkuta Mganga nyumbani kwake. Kwakuwa alikwenda na basi la timu, ilibidi wachezaji waende uwanja wa Taifa kwa miguu toka Hosteli ya Jeshi la Wokovu, Kurasini."
CHABANGA H. DYAMWALE
Meneja Uwanja wa Taifa, 1972.
(10.10.2016)


NB: Kutokana na fedheha hiyo kubwa, inasemekana Rais Nyerere alisusa kukanyaga tena mpirani!!

SWALI: Kuna mwingine anajua mengine zaidi ya hayo kuhusiana na Taifa Stars?

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic