January 10, 2017



Mshambuliaji Ibrahim Ajibu ni kati ya walio tayari kwa ajili ya mechi yao watani wao Yanga, leo.

Simba inaivaa Yanga katika mechi nusu fainali ya ya Kombe la Mapinduzi kwenye Uwanja wa Amaan mjini Zanzibar.

Ajibu ambaye amerejea nchini wiki iliyopita baada ya kufanya majaribio Haras El Hodood, ameanza mazoezi na wenzake na yuko tayari kwa ajili ya mechi ya leo.

“Ajibu naye yuko fiti, hapa ni chaguo la mwalimu Omog kama atamhitaji,” kilieleza chanzo.


Hata hivyo, kinachoonekana ni chaguo kubwa alilonalo Kocha Joseph Omog kwa kuwa pamoja na Ajibu, wako akina Mohamed Ibrahim, Pastory Athanas, Juma Luizio, Shiza Kichuya na wnegine wengi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic