January 5, 2017




Barua ikimuonyesha Mkurugenzi wa Habari wa Yanga, Jerry Muro akiomba kupunguziwa adhabu na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), imevuja mtandaoni.

Barua hiyo inaonyesha Muro aliandika Julai 7, mwaka jana akiomba kupunguziw aadhabu ya mwaka mmoja baada ya kuutumikia kwa miezi sita.

Muro alifungiwa na TFF kwa mwaka mmoja kwa madai ya utovu wa nidhamu.
Hivi karibuni, Mkurugenzi wa kitengo cha habari cha klabu ya Simba, Haji Manara alimuombea msamaha Muro na kuishauri TFF kumuondolea adhabu hiyo.
SALEHJEMBE, inamuunga mkono Muro kuomba radhi kwa kuwa ni sehemu ya uungwana wa mwanadamu kufanya jambo hilo.

SALEHJEMBE inaiasa TFF, kuliangalia ombi la Muro na ikiwezekana kulifanyia kazi kwa kumsamehe.




0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic