January 1, 2017

SIKU ALIPOONDOKA...


Farid Mussa amewasili katika visiwa vya Cannaries nchini Hispania tayari kuanza kazi katika kikosi cha Tennerife.

Timu hiyo ipo katika kisiwa cha Tenerife ndani ya visiwa hivyo vya Cannaries ambavyo viko karibu kabisa na nchi ya Morocco, Kaskazini mwa bara la Afrika.

Jose Thomas, mmoja wa viongozi wa mashabiki wa timu hiyo amesema Farid amepokelewa.

“Ndiyo amepokelewa, lakini sijafika kuona mechi wala mazoezini. Lakini ninaamini atakuwa ameanza kazi na kama bado basi baada ya mwaka mpya ataanza,” alisema.


Farid alichelewa kwenda Hispania kuanza kazi kwa madai ya kukosa kibali ingawa inaelezwa hakukuwa na suala la maelewano vizuri kati ya mawakala waliompeleka.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic