February 16, 2017


Mwenyekiti wa zamani wa Simba, Hassan Dalali amesema ni wakati mzuri wa kikosi cha Simba kuhakikisha inafanya vizuri zaidi na kubeba ubingwa.

Dalali ambaye sasa ni maarufu kama Trump amesema kwa kuwa Simba imerejea kileleni, inachotakiwa ni kuhakikisha haipotezi mchezo na itajihakikishia kubaki tena kileleni.

“Tulifikia pengo la pointi nane, tumepoteza hilo jambo ambalo ni baya. Lakini si wakati wa kujilaumu sasa, badala yake ni kupambana na kushinda kila mechi.

“Simba ikishinda kila mechi ni uhakika itarejea kileleni moja kwa moja na kubeba ubingwa,” alisema.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic