March 11, 2017



LICHA ya wachezaji wa Yanga kutolipwa mishahara ya miezi mitatu, lakini wamepanga kuingia uwanjani kwa nia moja tu pekee ya kuwafunga wapinzani wao Zanaco ya Zambia huku viongozi wao wakishughulikia tatizo hilo.


Timu hizo, zinatarajiwa kujitupa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam leo katika mechi ya hatua ya pili ya Ligi ya Mabingwa Afrika.


Mshindi wa mechi ya leo atafuzu hatua ya makundi na atakayefungwa atashushwa kucheza Kombe la Shirikisho Afrika akicheza mechi mbili za mtoano na timu za huko kuwania kufuzu Hatua ya Makundi Kombe la Shirikisho.


Chanzo kimeleza viongozi wa timu hiyo wanashughulikia mishahara hiyo na wakati wowote wanatarajiwa kulipwa.


Wachezaji hao walifanya kikao cha wao wenyewe mara baada ya kumalizika kwa mazoezi ya mwisho ya timu hiyo yaliyofanyika jana asubuhi kwenye Uwanja wa Taifa. 


Katika kikao hicho, wachezaji walionekana kupeana mioyo ya kijasiri huku wakiweka matatizo yao pembeni na badala yake kuhamasishana ili washinde kwenye mechi ya leo kabla ya kurudiana Lusaka, Zambia.

“Wachezaji wote tunatakiwa kuungana na tuwe kitu kimoja ili kuipambania timu yetu kwa lengo la kupata mtaji mkubwa wa ushindi kabla ya kurudiana nyumbani kwao.


“Ninaamini kuwa, kama tukishinda mechi hii viongozi watahamasika na kushawishika kutulipa mishahara yetu ya miezi mitatu, hivyo kila mchezaji atakayepata nafasi ya kucheza, basi anatakiwa kupambana ili tushinde mchezo huu,” alisikika mmoja wa wachezaji akizungumza hayo.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic