May 3, 2017



Uongozi Klabu ya Azam FC, umesema kuwa utautumia vilivyo udhamini wao kutoka Benki ya NMB kukijenga upya kikosi chao ili siku zijazo waweze kufika mbali kwenye michuano ya kimataifa.

Wikiendi iliyopita, Azam iliondolewa rasmi kwenye kinyang’anyiro cha kusaka tiketi ya kushiriki michuano ya kimataifa baada ya kufungwa na Simba bao 1-0 kwenye mchezo wa nusu fainali ya Kombe la FA.

Kwa muda wote ambao NMB imekuwa ikiidhamini Azam, timu hiyo imefanikiwa kubeba Kombe la Mapinduzi pamoja na Kagame pekee, lakini uongozi huo umesema kuwa kwenye vipengele vya mkataba kuna sehemu wanatakiwa kukuza soka la vijana na sasa watakitumia vyema.

Meneja wa Azam FC, Philipo Alando, amesema hayo hivi karibuni wakati wafanyakazi wa NMB walipotembelea makao makuu ya klabu hiyo maarufu kama Azam Complex jijini Dar na kushuhudia maendeleo mbalimbali yanayotokana na uwekezaji huo na kufanikiwa kucheza mechi moja ya kirafiki na kukubali kichapo cha mabao 7-2, kutoka kwa Azam U-20.

“Kiukweli mafanikio yetu yanatokana na udhamini wetu, licha ya uchanga wetu lakini tumeweza kupambana na timu kongwe za Simba na Yanga.

“Sasa baada ya kumudu ushindani wa ligi ya ndani, mikakati yetu kwa sasa ni kuhakikisha tunakijenga kikosi chetu kuwa imara zaidi ili siku zijazo tufike mbali,” alisema Alando.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic