May 1, 2017




Kiungo Mghana Sulley Muntari amekutana na tabia chafu na mbovu zinazopaswa kulaaniwa za baadhi ya wazungu wajinga kuamua kumbagua, jana.


Hali hiyo imemkuta katika mechi ya Ligi Kuu Italia maarufu kama Serie A wakati akiichezea Pescara dhidi ya Cagliari ambayo mashabiki wake ndiyo walimbagua Muntari ambaye baadaye alilazimika kutoka nje.



Muntari alilazimika kutoka nje baada ya kumfuata mwamuzi na kumueleza kilichokuwa kinatokea ili asimamishe mchezo kama sheria zinavyoeleza, lakini mwamuzi aligoma na kumpa kadi ya njano.


Kitendo hicho kilimuudhi zaidi na Muntari aliyewahi kung’ara na AC Milan, akaamua kutoka nje na kuiacha timu yake ikiwa na wachezaji pungufu uwanjani.



Baada ya kuona hivyo, meneja wa uwanja huo aliamua kutangaza kupitia spike za uwanja akiwaonya mashabiki hao kuacha ujinga huo.

Hii si mara ya kwanza kwa mashabiki wa Cagliari kuonyesha ubaguzi wa wazi, waliwahi kufanya hivyo kwa Samuel Et'oo mwaka 2010 wakati akiichezea Inter Milan, mwamuzi alisimamisha mchezo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic