August 4, 2017



Uongozi wa Yanga umetaka Bodi ya Ligi Tanzania (TPLB) kuwaomba radhi mara moja.

Yanga wametaka kuombwa radhi kutokana na kitendo chao cha kutoalikwa katika zoezi la kukabidhi vifaa lililofanywa na Kampuni ya Vodacom na wao hawakualikwa.

“Halikuwa jambo jema na pia linatuharibia kwa kuwa jezi zetu ni mkataba wetu na SportPesa na si Vodacom. Lakini ajabu hatukuambiwa wakati na sisi tulikuwa tumepanga jezi hizo zifanyie uzinduzi maalum na mchezaji wa zamani wa Arsenal, Sol Campbell ambaye anakuja nchini,” alisema Katibu Mkuu wa Yanga, Charles Boniface Mkwasa.


Wakati wa zoezi hilo, Msemaji wa Simba, Haji Manara alijitokeza kuwasaidia Yanga kupokea jezi, jambo ambalo limechangia kuibuka kwa hasira za Yanga ambao wameonyeshwa kukerwa na hali hiyo.

1 COMMENTS:

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic