August 12, 2017



TOFAUTI na miaka iliyopita ya rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kuapishwa siku chache baada ya uchaguzi lakini leo hapa Dodoma ambapo unafanyika uchaguzi, rais ataapishwa muda mfupi baada ya kushinda.



Uchaguzi Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) unafanyika leo mjini hapa kwenye Ukumbi wa St Gasper kwa ajili ya kuwapata washindi wa nafasi ya urais, makamu wa rais na wajumbe wa kamati ya utendaji.

Uchaguzi huo unasimamiwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya TFF, Wakili Revocatus Kuuli unafanyika baada ya Jamal Malinzi kuelekea kumaliza kipindi chake cha uongozi cha miaka minne.

Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Dr, Harrison Mwakyembe amesema hayo leo alipokuwa akizungumza na wajumbe wa mkutano mkuu na waandishi wa habari.

Mwakyembe amesema rais na wajumbe watakaopatikana leo wataapishwa mbele ya wapiga kura wote wa uchaguzi tofauti na miaka ya nyuma ambapo walikuwa wakishahau haki ya waliowachagua kwa kuwaapisha nje ya utaratibu.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic