September 29, 2017



Baada ya Ashanti United na Friends Rangers kuchuana leo Ijumaa, mechi nyingine za Ligi Dataja la Kwanza zitaendelea kesho Jumamosi Septemba 30, mwaka huu.

JKT Ruvu na Kiluvya United zinatarajiwa kucheza kesho kwenye Uwanja wa Mbweni katika mchezo wa kundi A kama ilivyokuwa kwa timu ambazo zimecheza leo - Ashanti na Friends.

Kundi B kutakuwa na michezo miwili ambako Mufindi United itacheza na Mlale JKT kwenye Uwanja wa Samora mjini Iringa wakati KMC itacheza na Coastal Union kwenye Uwanja wa Azam, Dar es Salaam.


Kundi C kutakuwa na mchezo mmoja ambako Rhino itacheza na JKT Oljoro kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic