September 9, 2017


FULL TIME

Dakika ya 93: Mwamuzi anamaliza mchezo, matokeo ni 0-0, hakuna mbabe.

Dakika ya 92: Presha ni kubwa ikiwa imesalia dakika moja.

Dakika ya 90: Zimeongezwa dakika 3.

Dakika 89: Mashabiki wanaonekana kuwa na presha, timu zote zinacheza kwa tahadhari.

Dakika ya 87: Simba wanaponea chupuchupu kufungwa baada ya shuti kali kupita pembeni kidogo ya lango.


Dakika ya 81: Simba wanafanya mabadiliko, anatoka Gyan anaingia Mohamed Ibrahim 'Mo'.

Dakika ya 81: Simba wanafanya mabadiliko, anatoka Gyan anaingia Mohamed Ibrahim 'Mo'.

Dakika ya 80: Simba wanafika langoni mwa Azam mara mbili mfululizo, lakini walinzi wa Azam wanakuwa makini.



Dakika ya 75: Kasi ya mchezo imepungua kiasi.

Dakika ya 70: Ndemla anapata nafasi ya kupiga shuti kali baada ya beki wa Azam kujichanganya, shuti linapaa juu ya lango.

Dakika ya 68: Simba wanafanya mabadiliko, anatoka Kichuya, anainfia Said Ndemla.


Dakika ya 67: Mchezo umebalansi kwa timu zote. 


Dakika ya 62: Mchezo unaendelea kwa kasi.



Dakika ya 60: Bocco anapiga shuti linadakwa.

Dakika ya 57: Azam wanafanya mashambulizi mawili ya nguvu, lakini Simba wanatulia na kupiga pasi.


Dakika ya 55: Yahaya wa Azam anapiga shuti linapita pembeni kidogo ya lango la Simba.


Dakika ya 50: Simba wanafika langoni mwa Azam lakini wanakosa umakini.


Dakika ya 49: Mbaraka Yusuf wa Azam anacheza faulo.


Kipindi cha pili kimeanza.

MAPUMZIKO


Dakika ya 47: Mwamuzi anakamilisha kipindi cha kwanza, timu zote zimeenda kupumzika.


Dakika ya 45: Mwamuzi anaonyeshga dakika mbili za nyongeza.


Dakika ya 41: Timu zote zinapokezana kumiliki mpira.


Dakika ya 40: Mchezo umepungua kasi lakini soka la nguvu limetawala.


Dakika ya 35: Yahaya wa Azam anagongwa na Mwanjali wakati wa kuwania mpira hewani, anaumia na kulala chini, anapatiwa matibabu.



Dakika ya 32: Azam wanafanya shambulizi kali, shuti la Yahaya linapanguliwa na Aishi Manula.

Dakika ya 26: Simba wanapata kona, anapiga Kichuya inadakwa na kipa wa Azam.


Dakika ya 24: Nahodha wa Simba, Method Mwanjali yupo chini, mchezo umesimama kwa muda, anapatiwa matibabu ya mguu.


Dakika ya 21: Mchezo ni mkali, umetawaliwa na mbinu nyingi.



Dakika ya 18: Azam wanapiga shuti kali nje ya boksi linadakwa na Aishi Manula.
Dakika ya 13: Azam wanatengeneza nafasi mara kadhaa, mchezo unakuwa na kasi, timu zote zinapiga pasi ndefu.

Dakika ya 10: Nahodha wa Azam, Himid Mao anapewa kadi ya njano kwa kucheza faulo.


Dakika ya 7: Mchezo umeanza kwa kasi, ushindani upo sehemu ya katikati ya uwanja.

Dakika ya 5: Simba wanafanya shambulizi kali, mpira wa kichwa unaokolewa na kipa wa Azam FC inakuwa kona.
Dakika ya 2: John Bocco wa Simba anapuliziwa filimbi kwa kuunawa mpira, analalamika akidai mpira ulimgonga kifuani.
Mchezo umeshaanza dakika ya kwanza.
Timu zote zimeshaingia uwanjani, muda wowote mchezo utaanza.
Huu ni mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara ambao utachezwa kwenye Uwanja wa Azam Complex maarufu kwa jina la Uwanja wa Chamazi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic