Wakati Barcelona ikiendeleza ushindi wa asilimia 100 katika Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa kuitwanga Olympiacos kwa mabao 3-1, Lionel Messi amefunga bao lake la 100 barani Ulaya.
Wakati Messi akifunga bao lake la 100 na kutoka uwanjani na furaha, beki Gerard Pique alitoka mapema baada ya kulambwa kadi nyekundu.
Messi amefunga mabao 100 katika mechi 122 na Cristiano Ronaldo ni mchezaji mwingine mwenye aliyewahi kufikisha idadi hiyo ya mabao baada ya kucheza mechi 143.
Messi alifunga bao hilo kwa mkwaju wa adhabu na kumfanya afikishe idadi hiyo.














0 COMMENTS:
Post a Comment