October 1, 2017



MPIRA UMEKWISHAA

-Mavugo anaachia mkwaju mkali kabisa, goal kick
-Aishi amesimama na mpira sasa unaendelea
-Aishi Manula yuko nje anatibiwa


DAKIKA 3 ZA NYONGEZA
Dk 90 Stand wanapoteza nafasi nzuri Manula akiwa nje ya lango, Kisatya anapiga shuti kali nje
Dk 89 Simba wanachofanya ni kuubakiza mpira katika himaya yao kwa pasi fupifupi, huku Stand wakiutoa nje kila mara
Dk 87, Bocco anapiga chenga mabeki wawili na kuachia mkwaju mkali, goal kick
SUB Dk 85 anakwenda nje Haruna Niyonzima na nafasi yake inachukuliwa na Jonas Mkude


Dk 84, kinachoonekana Simba wameamua kupiga mipira ya juu langoni mwa Stand ili kuwachanganya ikiwezekana wapate bao la pili. Lakini pia wachezaji wa Simba wanaonekana kupoteza muda
Dk 83, Simba wanafanya shambulizi, Niyonzima anapaishaa juuu
KADI DK 81 kadi ya kwanza ya njano inakwenda kwa Stand
Dk 79, Manula anafanya kazi ya ziada kuokoa mpira wa adhabu na kuwa kona, Stand wanachonga lakini haina faida
SUB 76 Sixtus Sabilo anaingia, SABILO Kitoba Emmanuel amekwenda nja upande wa Stand
Dk 75, Mbonde anaanchia mkwaju mkali kabisa hapa, goal kick
Dk 70, Bocco anatpa pasi nzuri kwa Kichuya lakini shuti lake linakuwa nyanya hapa

SUB Dk 69 Mageta Mirambo anaenda nje, kaingia Kisatya Sahani anaingia upande wa Stand
SUB Dk 68, Simba wanamtoa Muzamiru, anaingia Said Ndemla
Dk 67, nafasi nzuri Simba, Mavugo anabaki yeye na kipa baada ya pasi ya Bocco, anapiga, kipa anaokoa, kona
DK 65, Niyonzima anapiga mkwaju wa faulo, goal kick
Dk 63, Nyoni katika nafasi nzuri kabisa, lakini anapiga juuu
DK 60, Stand wanajitahidi na wanaanza kubadilika wakicheza. Inaonyesha bao morali
Dk 58 Mavugo anafunga hapa akiunganisha krosi ya Nyoni, mwamuzi anasema weka kati, mwamuzi msaidizi anasema OFFSIDE
DK 54, nafasi nyingine kwa Stand lakini nafasi ya Mageta, anapiga nje


Dk 53, Simba wanapata kona, inachongwa vizuri na Niyonzima lakini kipa Stand anaokoa vizuri hapa
GOOOOOOOOO Dk 52, Mtasa anapiga Manula anapangua, anauwahi na kufunga bao la kwanza kwa Stand
Dk 51, Ally Shomari anashika ndani ya eneo la harati, PENAAAAAAT
Dk 47, Salamba anageuka vizuri mbele ya Mbonde, anaachia mkwaju safi kabisa, Manula anadaka
GOOOOOOOOOOO Dk 46, Mavugo anatulia ndani ya na kufunga vizuri kabisa
Dk 45, Kipindi cha pili kimeanza, Stand wakitaka kusawazisha na Simba wamepania kuongeza
SUB Dk 45 Simba wanamtoa Okwi na nafasi yake inachukuliwa na Laudit Mavugo


MAPUMZIKO

DAKIKA 2 ZA NYONGEZA

Dk 45, Bocco anaachia mkwaju mkuuubwa, goal kick
Dk 44 Okwi alijaribu kuwachambua mabeki wa Stand lakini Rajab anamuweka chini
Dk 43, krosi ya Mgeta inamgonga Salamba na mpira unatoka sentimeta chache nje ya lango la Simba, goal kick
Dk 40, Muzamiru anapokea pasi ya Kotei anaachia shuti, goal kick
Dk 36, Kichuya anaingia vizuri, krosi, Bocco anageuka na kuachia mkwaju, goal kickDk 35 kona inachongwa na Haruna, kipa anaokoa Bocco anataka kuwatoka mabeki, wanaondosha


Dk 34 Okwi anaingia vizuri lakini Rajab analala na kuokoa, kona. Inachongwa na Kichuya, Stand wanaokoa, kona tena
Dk 33, kona inachongwa hapa lakini Stand hawakujipanga vizuri
Dk 32, Manula anaruka na kuokoa vizuri kabisa mkwaju wa faulo na kwua kona
Dk 28, krosi ya mpira wa adhabu ya Okwi unapita juuuuu ya lango la Stand
Dk 25, pasi nzuri anapokea Okwi ndani ya 18 ya Stand lakini mwamuzi anasema ni goalkick
Dk 23 Kotei anagongana na Salamba, yuko chini anatibwa 
GOOOOOOOOOO Dk 17, Kichuya anaachia mkwaju mkali nje ya 18 baada ya pasi ya kichwa ya Bocco


Dk 14 sasa, bado mpira hauna ladha sana kutokana na ubovu wa uwanja ingawa Simba wanaonekana kufunguka na kucheza pasi
Dk 11, Okwi anatoa pasi nzuri kwa Niyonzima lakini mpira unamzidi spidi
Dk 10 sasa, mpira zaidi unachezwa katikati ya uwanja
Dk 7, Salamba anageuka na kuachia mkwaju hapa lakini unapaa juu
Dk 5, mpira wa kurusha wa Kibopile, Manula anautema lakini Simba wanaondosha eneo la hatari
Dk 4 sasa, bado mpira haujachangamka na uwanja unaonekana kuwapa wachezaji wakati mgumu
Dk 1, Bocco anaruka juu na kupiga kichwa lakini kipa anadala kwa ulaini kabisa

Dk 1, mpira umeanza na Simba ndiyo wanakuwa wa kwanza kufika langoni mwa Stand

2 COMMENTS:

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic