October 23, 2017



Pamoja na taarifa kama Yanga itaweka kambi mjini Morogoro umeonyesha kuendelea kufanya siri jambo hilo.

Taarifa za Yanga kuweka kambi mjini Morogoro kujiwinda dhidi ya Simba Agosti 28 zilianza juzi lakini uongozi wa Yanga kutotaka kuliweka hadharani jambo hilo.

Msemaji wa Yanga, Dismas Ten amesisitiza kwamba watatangaza kambi yao ilipo baada ya kufika Dar es Salaam.

“Kwa sasa tuko Shinyanga, tutakapofika Dar es Salaam tutatangaza kambi yetu ni wapi, si sasa,” alisema.

Taarifa nyingine zinaeleza, Kocha George Lwandamina alivutiwa na kambi ya Morogoro ambayo aliitumia kujiandaa wakati wa Pre Season.

“Kocha aliipenda sana kambi ya Morogoro, utulivu na hali ilivyo. Nina uhakika kocha atataka Morogoro,” kilieleza chanzo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic