February 13, 2018

AFRICAN LYON MSIMU ULIOPITA



Mechi namba 53 Kundi A (Kiluvya United 0 vs African Lyon 1). Klabu ya African Lyon imepigwa faini ya sh. 200,000 (laki mbili) kutokana na timu yake kutoingia vyumbani katika mechi hiyo iliyofanyika Februari 5, 2018 kwenye Uwanja wa Filbert Bayi mkoani Pwani.

Kitendo hicho ni ukiukaji wa Kanuni ya 14(13) ya Ligi Daraja la Kwanza kuhusu Taratibu za Mchezo. Adhabu hiyo imetolewa kwa kuzingatia Kanuni ya 14(49) ya Ligi Daraja la Kwanza kuhusu Taratibu za Mchezo.


Mechi namba 53 Kundi B (Mawenzi Market 0 v Coastal Union 2). Klabu ya Mawenzi Market imepigwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) kutokana na washabiki wake kuwarushia chupa Waheshimiwa Mawaziri ambao ni washabiki wa Coastal Union katika mechi hiyo iliyofanyika Februari 2, 2018 kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic