February 22, 2018




Na George Mganga

Rais wa Shirikisho la Soka Duniani (FIFA), Gianni Infantino, amepokelewa na ngoma za kiasili kutoka kwa kabila la Wamasai, ambao walimbatana na zawadi mbalimbali za kiasili.

Infantino alipokea zawadi hizo leo mapema, kabla ya kufungua mkutano wa FIFA Excutive Summit, katika ukumbi wa JNICC jijini Dar es Salaam.

Infantino amewasili hapa akiwa na viongozi wengine mbalimbali, ikiwemo Rais wa CAF, Mr. Ahmad, kwa ajili ya mkutano wa mwaka wa FIFA unaoanza leo February 22.

Ujio wa Rais huyo ni maalum kwa ajili ya majadiliano kuhusu Soka la Wanawake, Vijana, Mipango ya kukuza soka kwa nchi za Afrika, pamoja na kusaidia vilabu kujiendeleza kisoka kiujumla.

Infantino ataondoka nchini mara tu baada ya mkutano huo kumalizika.

Tazama hapa namna alivyopokelewa na kabila la Wamasai waliombatanisha zawadi mbalimbali kwake.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic