April 26, 2018



Usiku wa Ulaya unaendelea tena leo katika UEFA Europa Ligi ambapo klabu ya Arsenal itakuwa kwenye uwanja wake wa nyumbani kucheza dhidi ya Atletico de Madrid ya Spain.

Arsenal inaanza kutupa karata yake ya kwanza kufuatia kutinga hatua ya nusu fainali ya mashindano hayo kwa kuiondosha CSKA Moscow ya Urusi kwa jumla ya mabao 4-1.

Kikosi hicho cha Arsenal kilipangwa kucheza na Madrid kufuatia droo ya makundi kufanyika baada ya 16 bora kumalizika.

Mechi hiyo itaanza majira ya saa 4 na dakika 45 usiku wa leo katika Uwanja wa Emirates.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic