April 21, 2018

Enyimba FC


Na George Mganga

Droo ya upangaji wa timu zitakazokutana hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika inatarajia kufanyika Jumamosi ya leo Aprili 21 2018.

Jumla ya timu 16 zimeshatinga kuingia hatua hiyo baada ya michezo 16 kupigwa ndani ya wiki hii.

Yanga kutoka Tanzania ni timu pekee inayotuwakilisha kimataifa nayo imetinga hatua hiyo baada ya kuiondoa Wolaita Dicha SC kutoka Ethiopia kwa idadi ya mabao 2-1.


Licha ya kukubali kichapo cha bao 1-0 ugenini mjini Awassa, Ethiopia, Yanga ilifanikiwa kusonga mbele kutokana ushindi wa mabo 2-0 ilioupata kwenye Uwanja wa nyumbani jijini Dar es Salaam.
Timu zilizofuzu kuingia hatua hiyo ni zifuatazo

1. Williamsville (Ivory Coast)
2. Asec Mimosas (Ivory Coast)
3. RajaCasablanca (Morocco)
4. Berkane (Morocco)
5. USM Alger (Algeria)
6. Al Masry (Egypy)
7. Carabrazavile (Congo)
8. AS Vita (DRC)
9. Young Africans SC (Tanzania)
10. GorMahia FC (Kenya)
11. Rayon Sports (Rwanda)
12. Al Hilal(Sudane)
13. Djoliba (Mali)
14. Aduana Stars (Ghana)
15. Enyimba (Nigeria)
16. UD Songo (Mozambique)

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic