April 25, 2018



Zikiwa zimesalia siku tano pekee kueleka mechi ya watani wa jadi, Simba na Yanga, Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limetangaza kuimarisha zaidi ulinzi.

Kwa mujibu wa Afisa Habari wa TFF, Clifford Ndimbo, amesema kuwa jumla ya Camera 109 zitafungwa Uwanjani kuelekea mechi hiyo inayoteka hisia za mashabiki na wadau wa soka nchini.

Clifford ameeleza kuwa Camera hizo zitafungwa ili kuimarisha ulinzi na usalama ndani ya Uwanja ambapo zitakuwa zinarekodi matukio mbalimbali kabla na baada ya mchezo.

Mechi hiyo inatarajiwa kupigwa Aprili 29 2018 katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.

Tiketi za mchezo huo zimeshaanza kuuzwa kupitia Selcom na kwale wote ambao hawajanunua wanaweza kuzipata muda wowote.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic