June 12, 2018


Na George Mganga

Rasmi uongozi wa Azam FC umemtambulisha aliyekuwa Mshambuliaji wa Njombe Mji, Ditram Nchimbi, baada ya kuingia naye mkataba wa miaka miwili.

Nchimbi amejiunga Azam akitokea Njombe Mji iliyoteremka daraja katika msimu uliopita wa Ligi Kuu Bara.

Ujio wa Nchimbi ndani ya kikosi cha Azam umezidi kuongeza wachezaji wapya watakaokuwa na timu hiyo msimu ujao baada ya usajili wa Donald Ngoma na Tafadzwa Kutinyu.

Mchezaji huyo ataungana na wenzake hivi karibuni tayari kuanza mazoezi kwa ajili ya mashindano ya Kagame yanayotarajia kuanza Juni 28 mwaka huu.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic