June 11, 2018


Benki ya NBC imemshitaki Mfanyabiashara na aliyekuwa Mwwenyekiti wa klabu ya Yanga, Yusuf Manji kwa kushindwa kulipa mkopo wa shilingi bilioni 26.

Taarifa kwa mujibu wa gazeti la Dailu News limeeleza kuwa Manji amekuwa miongoni mwa wafanyabiashara hao wakiwemo wengine wanne wanaodaiwa kiasi hicho cha fedha.

Daily News liemandika kuwa NBC wamemfungulia Manji mashitaka na wenzake katika Mahakama Kuu, Divisheni ya Biashara ambapo madai ya kwanza ni juu ya Farm Equip (Tanzania) Company Limited, na Manji na watu wengine wanaosimama kama wadhamini.

Wadaiwa wengine katika mkopo huo ni pamoja na Tanperch Limited, Quality Group Limited na Kaniz Manji. Mkopo wa pili ulikwenda kwa Tanperch Limited, ikiripotiwa umedhaminiwa na Manji, Quality Group Limited na Kaniz Manji, ambao pia ni wahusika.

Daily News wamednaika wakieleza kwa mujibu wa brua iliyochapishwa kwenye vyombo vya habari hivi karibuni, imeeleza washitakiwa hao wanatakiwa kuwasili mahakamani wao wenyewe au watume mawakili wao Juni 25 2018 kesi hiyo itakaposikilizwa.

Wakati wakuchukua mikopo hiyo, mali zisizohamishika pamoja na mejengo ziliwekwa kama dhamana ikiwa na pamoja na viwanja vitatu vilivyopo jijini Mwanza, Ilemela.

Jengo la Quality Group Limited ni miongoni mwa mali zilizowekwa kama dhamana na endapo mkopo hautarudi litawezwa kupigwa mnada ili kufikidia madeni ya madeni ya Farm Equip (Tanzania) Company Limited.


17 COMMENTS:

  1. Kaka hii sio habari ya michezo, chuki zako zitakufanya ufe kwa pressure bila maendeleo yoyote. Najua hukupenda matokeo ya mkutano wa Jana Ila ndo hivyo. Mnafiki hajifichi, we ni miongoni mwa wachawi wa Yanga. Mfanya biashara kudaiwa ni issue za kawaida sana. After all sijui kama unajua hata source ya mgogolo wao. Ulikuwa wapi usiandike hadi Leo, wachawi tumeshawasikia na kuwaona sana. Ila yanga ni timu ya wananchi siku zote itashinda na mtaona aibu

    ReplyDelete
    Replies
    1. Sema imekugusa tu kama Mwana yanga.... Kwani Akina malinzi Kuwa lupango ni habari za michezo? Ukikubali Manji ni mwenyekiti wa yanga basi ni mwanamichezo na watampost tu huwezi zuia

      Delete
  2. Mtu kashindwa kulipa deni vipi yanga wamsakame kuibeba timu hiyo. Ikowapi huruma hapo. Manji sie yule wazamani mwacheni apumuwe

    ReplyDelete
  3. Acheni uandishi kasuku na chuki binafsi sisi tunatanaka habar za Michezo sio za watu binafsi

    ReplyDelete
  4. Mi naona Manji anataka yanga imtimizie malengo na sio yeye kuisaidia yanga sema njaa ikiingia.....

    ReplyDelete
  5. Hiyo ni habari ya michezo. Habari yoyote inayomhusu mwanamichezo ni ya kimichezo mbona wachezaji wakifiwa ikaripotiwa humu hakuna anaye bwabwaja

    ReplyDelete
    Replies
    1. MO alihusika katika utapeli wa mafuta kiwanda chake cha Bidco mbona sijaona popote kurasa za michezo imewekwa?

      Delete
  6. Hii habari ilitakiwa kuandikwa kwenye gazeti la Mwananchi.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Hilo jamaa no fala eti, amekopi kwa mjinga mwenzie binzubeiry, wanaumia sana manji kuwa yanga. Bill.26 kwan nn au anadhani anafanya biashara za kuchoma miguu ya KUKU? Wajinga hawa wapo watatu huyu chwupe dawa kipara na lile ginia la mkaa. Ila kwa mwaka huu watapambana na halo zao

      Delete
  7. Hats mnada ukiwa Leo utanunu nini mjinga ww,

    ReplyDelete
  8. Hee ajabu. Mnapinga hadaiwi au NBC wamezua?Di not kill the messengers. Hao wameripoti tu.Waulizeni Daily News habari Hai wameipata wapi?Au mlitaka NBC wasamehe deni lao?

    ReplyDelete
  9. Don't overwhelm Manji especially during this period of acute economic situation he is facing. Manji has done a lot for yanga and desperately needs mercy, not tension and disturbance. Let him find means to solve unexpected situation he is facing.

    ReplyDelete
  10. Kutokana na hali aliyokuwa nayo Manji na kutokana ukarimu wake usiokuwa na mpaka juu ya Yanga na kwa asante anayostaki, Yeye ndie anaestahaki msaada wa kujikwamuwa badala ya yeye kushinikzwa kuinusuru Yanga. A friend in need, is a friend indeed

    ReplyDelete
  11. Manji aliuweka utajiri wake wote ndani ya mikono ya yanga na leo, haya ndio yaliyomfika na bado anaandamwa jamaa wanataka hela, eti wote wamelikataa ombi la kujienguwa

    ReplyDelete
  12. Yaani mkisikia Manji tu chupi zinawabana Saleh usisahau mtu mbaya Bin Kleb karudi huyo ni mbaya sana aliwafanyia kitu kibaya sana Rwanda wewe na Rage kumsajili Mbuyu Twite.

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic