January 30, 2021

 


OFISA Habari wa Ruvu Shooting inayoshiriki Ligi Kuu Bara amewaomba Watanzania wamuombee kwa kuwa kwa sasa hali yake haijatengamaa kwa kile ambacho ameambiwa na madaktari kuwa amekula chakula chenye sumu.

Kupitia ukurasa wake wa Istagram Masau Bwire ameandika:Kwa siku kadhaa zilizopita, nimekuwa sipokei simu, au nikipokea nasema tu siko vizuri, siwezi kuzungumza! Wapo walionielewa, lakini wapo walioona kama ni jeuri na kiburi tu, nafanya makusudi, kwa sababu sitaki kuzungumza nao.


Niwaombe radhi, wanisamehe kwa yote, lakini pia niwaaambie, na kuwahakikishia kwamba, sina kawaida hiyo ya kutopokea simu ya mtu yeyote atakayenipigia, siwezi kudharau simu ya mtu yeyote, daima namuomba Mungu, aniepushe na tabia hiyo ya kishetani ya kudharau na kutowapa ushirikiano pale wanapohitaji lolote kutoka kwangu.

Kwa kweli nilikuwa katika hali ngumu, kama unavyoiona hiyo picha, ndio uhalisia wa namna nilivyokuwa, nilikamatika haswa! Baada ya vipimo vya Hospitali, wataalamu wa afya (Daktari), walinambia, nilikula chakula ambacho hakikuwa salama,  chenye sumu!

Mwili pamoja na kwamba, haujawa na nguvu ya kutosha, hata kazini bado sijaweza kwenda, namshukuru Mungu, kwa kweli sijambo, naendelea vizuri.


Nikumbukeni katika maombi.

15 COMMENTS:

  1. Pole sana na Mwenyezi Mungu akuponye

    ReplyDelete
  2. Pole sana kiongozi Mungu akupe wepesi upone haraka

    ReplyDelete
  3. Pole mwanampira mwenzetu. Mungu akuponye

    ReplyDelete
  4. Pole Sana Msemaji.
    Mungu atakuponya tena kutoka kindani

    ReplyDelete
  5. Kiki tu hiyo Mgonjwa ana simu kwenye paja??

    ReplyDelete
  6. Pole sana, ila punguza kula mihogo pori

    ReplyDelete
  7. HILI JAMAA NI PUMBAVU SANA WATU HAWAJAGUNDUA TU

    ReplyDelete
  8. Nakubaliana na wewe Anapenda kiki tu Angalia hiyo picha kwa makini.Ipi staged.Ni ya kupanga.Simu kwenye paja.Alivyolala.

    ReplyDelete
  9. Sasa nyie mikia fc imekuwaje tena kutaka kumtoa roho mzee wa kupapasa>?

    ReplyDelete
  10. Wewe mbwa una ushahidi wa hayo unayosema?Utopolo ukiitwa kutoa ushahidi utaweza kuutoa.TCRA kutoa IP ya simu au Internet iliyotumika kuandika huu uzushi utajibu nini?
    Utopolo wakati mwingine kaa kimya.

    ReplyDelete
  11. Sasa huyu naye kuna mtu anashida nae hadi ahangaike kumtoa roho? Uroho wake ndip umemfanya afakamie vyakula vyenye viwango cha chini ndio yakampata hayo kama ni kweli anyway

    ReplyDelete
  12. Ni kiki tu hamna lolote.Mtu wa kawaida hatembei na simu 6.

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic