Kagere ametua Simba hivi karibuni akitokea Gor Mahia ya Kenya ambayo mashabiki wao mpaka leo hawaamini kilichotokea mpaka akawakimbia. Amefunga mabao manne kwenye Kagame.
Raia huyo wa Rwanda ambaye jana Jumamosi aliondoka kwenda kwao kukamilisha mambo yake amesema; “Unajua asilimia kubwa ya wachezaji wengi ambao tulikuwa tunacheza ndiyo mara yetu ya kwanza kuwa hapa sasa imechangia kwa namna fulani hivi kushindwa kupata kile ambacho tunakitaka kwenye Kagame.”
Meddie Kagere.
Kocha wa Simba, Masoud Djuma aliwapa mapumziko wachezaji waliotumika kwa asilimia kubwa kwenye ligi wakiwemo Okwi, Bocco, Aishi Manula, Haruna Niyonzima, Jonas Mkude na wengineo.









0 COMMENTS:
Post a Comment