September 27, 2018


Na George Mganga

Kocha Mkuu wa timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' Emmanuel Amunike, ametangaza kikosi cha wachezaji 30 watakoacheza mechi ya kufuzu AFCON 2019 dhidi ya Cape Verde Oktoba 12 2018

Magolikipa

1. Aishi Manula (Simba)
2. Mohamed Abdulrahman (JKT)
3. Benno Kakolanya (Yanga)

Mabeki

4. Shomary Kapombe (Simba)
5. Hassan Kessy (Nkana, Zambia)
6. Salum Kimenya (Tz Prisons)
7. Gadiel Michael (Yanga)
8. Paulo Ngalema (Lipuli)
9. Ally Sonso (Lipuli)
10. Kelvin Yondani (Yanga)
11. Abdi Banda (Baroka, Afrika Kusini)
12. Abdallah Kheri (Azam)
13. Agrey Morris (Azam)
14. Andrew Vincent Dante (Yanga)
15. David Mwantika (Azam)

Viungo 

16. Himid Mao (Pertojet, Misri)
17. Jonas Mkude (Simba)
18. Mudathir Yahya (Azam)
19. Feisal Salum (Yanga)
20. Frank Domayo (Azam)
21. Saimon Msuva (El Jadidi, Morocco)
22. Farid Mussa (CD Tenerife, Hispania)
23. Salum Kihimbwa (Mtibwa)

Washambuliaji

24. Mbwana Samata (Genk, Ubelgiji)
25. John Bocco (Simba)
26. Thomas Ulimwengu (A Hilal, Sudani)
27. Rashid Mandawa (BDF XI, Botswana)
28. Yahya Zayd (Azam)
29. Shaban Chilunda (CD Tenerife, Hispania)
30. Kelvin Sabato (Mtibwa Sugar)

12 COMMENTS:

  1. Wapi Ibrahim Ajibu, Kichuya na Nyoni.

    ReplyDelete
  2. Hata ajibu hayupo duh na kichuya kweli zama zimebadilika

    ReplyDelete
  3. huyu coach anajua tazama selection yake kaleta wacheza 9 toka nje ambao ni prossional players na kachukua wachezaji 21 toka timu saba (7) zinazocheza ligi kuu !! makocha wetu wangetujazia wachezaji wa Simba na Yanga tu lakini kachukua 6 toka azam na 5 yanga na 4 toka Simba Jkt mmoja Lipuli wawili Prison mmoja na Mtibwa wawili - very good combination

    ReplyDelete
  4. Combination nzuri ya timu haichaguliwi kwa mfumo wa kisiasa kwamba eti kila timu lazima itoe mchezaji au kwa idadi ya wachezaji sawa bali kwa ubora wa uchezaji. Kocha mzuri awezi hata kidogo akamuacha Ibrahim Ajib akiwa katika ubora huu na kumchukua Ally Sonso ambaye bado mchango wake huko Lipuli sio hata nusu ya mchango aliotoa SALAMBA. Ajabu sana. Anawezaje kumuacha Erasto Nyoni akiwa katika ubora wake na kumchukua Abdallah Kheri wa Azam ambaye hata Azam kwenyewe hayuko first eleven? Kwa Kichuya sitaki kumuongelea maana kila mmoja anajua kazi na umuhimu wake katika timu ya taifa. Kumbuka mechi yake ya mwisho stars dhidi ya DRC iliyokuwa imesheheni wa kulipwa. Kocha wa DRC aliuliza kama Kichuya ni wa kimataifa maana aliupiga mwingi na hata kwenye klabu yake ni chagua la kwanza.

    ReplyDelete
  5. Kocha anaangalia fitness ya mchezaji dk 90, na uwezo wake wa kukaba akipokonywa mpira, Migomba ana kipaji ila pumzi inawahi kata na uwezo wake wa kunyang'anya mipira ni mdogo

    ReplyDelete
  6. KOCHA TUAMBIE LEO HII WACHEZAJI WAENDE KAMBINI WAPI MZEE TUSIRUDIE UTOVU WA NIDHAMU TIMU YA TAIFA KWANZA VILABU BAADAE SANA. KURIPOTI LEO SAA NGAPI MWISHO?

    ReplyDelete
  7. Kocha umefanya makosa kumuacha kichuya kwani ilibidi winga sumbugu namba 7 Msuva namba 11 Kichuya hapo ingepende xana

    ReplyDelete
  8. Tukisema mtarudishia ya usimba na uyanga lakini ukweli tupu huo wanaousema wengine - KICHUYA, AJIBU, ERASTO NYONI.

    ReplyDelete
  9. Kimsimgi kuna wachezaji wameitwa ili kukamilisha idadi lakini sio kuleta ushindani wa namba ndani ya stars. Kuwaacha wachezaji wa Simba na Yanga kwa sababu ya kuepuka usimba na uyanga japo kuwa wanauwezo huo ni ujinga.Waganda licha ya Juuko kutoichezea timu yake kwa kipindi lakini hawakuawacha kumuita cha msingi ukiacha wachezaji wanaocheza nje ni timu tatu nchini Azam,Yanga na Simba ndio timu zenye wachezji amabo wanauzoefu na mechi za kimataifa na wameshasafiri nchi kadhaa na wameshapata changamoto za makocha kadhaa wa kigeni wenye uzoefu kwa hivyo kupanga ni kuchagua kila la kheri stars.

    ReplyDelete
  10. This comment has been removed by the author.

    ReplyDelete
  11. kocha kama umeshindwa bara usema sisi tunataka ushindi na si maneno.

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic