JINA LA KLABU MPYA YA BECKHAM LATAJWA
Klabu ya David Beckham ya ligi ya Major League Soccer team nchini Marekani sasa itapatiwa jina la Club Internacional de Futbol Miami - ama Inter Miami CF - na tayari chapa ya klabu hiyo imezinduliwa.
Inter Miami itaanza kucheza katika ligi ya MLS 2020 baada ya kupewa kandarasi ya kuendelea mnamo mwezi Januari.
Chapa hiyo ina rangi ya waridi, nyeusi na nyeupe, ikishirikisha jua lenye miale saba. Hii ni siku nzuri kwangu na timu yote, alisema Becham.
Mchezaji huyo wa zamani wa manchester United, Real Madrid, Paris St Germain pamoja na AC Milan ambaye ni mmiliki na rais aliongezea: Tunachukua hatua nyengine muhimu kuimarisha klabu yetu na leo ni siku muhimu katika historia ya klabu ya Club Internacional de Futbol Miami."








0 COMMENTS:
Post a Comment