September 29, 2018


Ni kweli Yanga ni mabingwa mara 27 Tanzania huku Simba ikuchukua mara 19.

Ila kwa makombe yote Tanzania na yale vilabu vyetu vimewahi kushiriki Simba imechukua Makombe 51 huku Yanga ikiwa na 42.

Lakini tuwe wakweli kidogo, kwanini Simba baada ya kuchukua ubingwa msimu uliopita wenzetu wameamua kujiita Mabingwa wa kihistoria?

Hivi Tanzania na nchi zote za Afrika Mashariki na kati ipi kubwa ya Simba na Yanga? 

Simba ni Bingwa wa kihistoria wa ukanda huu wa Afrika, mbona sisi hatujiiti Mabingwa wa kihistoria wa zaid ya nchi 11? 

Yaani sisi ni Mabingwa wa Mabingwa wa kihistoria. Haya njoeni na FACTS na mapovu.

Hivi mshawahi kusikia Manchester United au Mufurila Wonderes ya Zambia wakijiita Mabingwa wa kihistoria? BINGWA NI MMOJA TU. HAKUNA WA KIHISTORIA WALA JIOGRAFIA

Na Haji Manara (Ofisa Habari wa klabu ya Simba)

5 COMMENTS:

  1. Hahahaa....hapo Manara Umenena.nawashangaa Yanga kujiita mabingwa wa kihostoria... sijui Bayern Munich wajiite mabingwa wa nini?

    ReplyDelete
  2. Mabingwa wa kihistoria wapo tu miaka nenda miaka rudi. Brazil na world cup, Real madrid na uefa champions league etc. So kwa yanga ni sahihi wao kujiita hivo...

    ReplyDelete
  3. Kwa hiyo Simba ni mabingwa wa kihistoria wa Afrika Mashariki na Kati na sio wa nchi moja tu.Au mantiki hiyo haifuatwi hapa?Jina hilo limezuliwa baada ya kupokwa ubingwa wa Tanzania.

    ReplyDelete
  4. Hapa Simba Atakuwa Bingwa wa vikombe wakati yanga akibaki kuwa wa historia

    ReplyDelete
  5. Wakosaji wote huwa wanajifariji.Yanga kama Manchester United wamebakia kusema ohh sisi wa historia.

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic