September 28, 2018


Na George Mganga

Kikosi cha Yanga jana kimeendelea kujifua na mazoezi mahususi ya kuandaa dozi maalum dhidi ya Simba katika mchezo wa Ligi Kuu Bara utakaofanyika Septemba 30 kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Katika mazoezi hayo Kocha Mkongomani, Mwinyi Zahera, alionekana kuwapa mazoezi ya pumzi wachezaji wake ikiwemo kukata upepo ili kuhakikisha wanaihimili Simba vilivyo.

Zahera amezidi kukifua vema kikosi chake ambacho kimeweka kambi maalum mjini Morogoro, sehemu ambayo utulivu wa aina yake ili kuwaandaa vema wachezaji kwa mechi hiyo kubwa.

Unaambiwa Zahera amewaongoza wachezaji kwa kutengeneza muunganiko mzuri haswa sehemu ya kiungo pamoja na safu ya ushambuliaji, huku akimpa nafasi Tambwe ya kuhakikisha anafanya maangamizi siku hiyo.

Kocha Zahera anaamini Tambwe atafanya vizuri baada ya kuisaidia Yanga kuibuka na ushindi wa mbao 2-0 dhidi ya Singida United kwenye mchezo wa mwisho wa ligi uliofanyika Uwanja wa Taifa, Dar.

3 COMMENTS:

  1. Kiukweli kabisa huwezi tafuta au pata pumzi kwa siku 3 au 5...utaniambia kama siyo kuona wachezaji wachovu wote

    ReplyDelete
  2. labda kawajaza kwa pampu

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic