September 18, 2018


Imeelezwa kuwa Kocha Mkuu wa Yanga, Mwinyi Zahera, jana aliwaondoa wachezaji wake watatu kwenye ratiba ya mazoezi kambini baada ya kushindwa kufuata masharti yake.

Wachezaji ambao ni Pius Buswita, Haji Mwinyi na Juma Makapu, walliondolewa na Zahera baada ya kushindwa kuonekana jukwaani kutazama mchezo wa timu yake dhidi ya Stand United.

Kocha huyo aliwalazimu wachezaji hao wautazame mchezo huo jukwaani lakini badala ya hawakufanya hivyo hivyo ikamlazimu awaondokea kambini kwenye mazoezi ya jana.

Kikosi cha Yanga kinaendelea na mazoezi hivi sasa kujiandaa na mechi za ligi kuu ikiwemo dhidi ya Coasta Union kesho kwenye Uwanja wa Taifa.


2 COMMENTS:

  1. UKALI UKIZIDI SANA TUTAHARIBU TIMU> SISI TUNAANZA KUIENGA UPYA MORALI YA TIMU YETU BAADA YA KUONDOKEWZ NA MFADHILI WETU NA MWENYEKITI WA KLABU. SASA MORALI YA WACHEZAJI IPO JUU HATA KESHO TUCHEZE NA WATANI WETU TUNAWEZA KUPIGA BAO TENA UZURI TUNAFUNGA MABAO MENGI SIKU HIZI. SASA KOCHA AENDE NAO WACHEZAJI TARATIBU.

    ReplyDelete
  2. Kweli kabisa, Kocha Zahera ajifunze kuzoea mazingiea, wachezaji wetu hawa ni wa kuwapeleka mdogo mdogo, adhabu ya utovu wa nidhamu kama kuchelewa mazoezi siyo lazima iwe kugukuza! Anaeza kujaribu njia mbadala kama faini za kjkata posho. Ukimfukuza mchezaji hata timu inakisa huduma yake, mnapoteza wote na mbaya zaidi mchezaji atalipwa tu. Mfano wa juzi kuacha kumpanga Kakolanya kuliigharimu timu lakin angekatwa posho ingekula kwake tu.
    Zahera aelewe hapa ni bongo kuna itikadi zake, ajenge umoja wa timu na morali, makicha wenzie wakali sana walichemsha mapema kweupe.
    Namshauri ayazingatie haya na kama mlezi aache nongwa, pasi na kupepesa macho Kamusoko mbovu hawezi kuwa sawa na Loti au Buswita.
    Wabillah taufiq

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic